Monday, August 12, 2013

Under Construction!

Mdau wa Theeastafrica alijichimbia.

Tuesday, November 27, 2012

LOWASSA AONGOZA HARAMBEE KUCHANGIA UJENZI WA BWENI LA WATOTO WA KIKE TEOFILO!

Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiongoza harambe ya kuchangia ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike katika Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji, kinachomilikiwa na Kanisa la Moravian nchini Tanzania,Jimbo la Kusini Magharibi,usharika wa Ruanda mjini Mbeya.Katika Harambee hiyo,Mh. Lowassa pamoja na marafiki zake wakiweza kuchangia sh millioni 25 kusaidia ujenzi huo.
Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiendesha harambe ya kuchangia ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike katika Chuo Kikuu cha
Teofilo Kisanji, kinachomilikiwa na Kanisa la Moravian nchini
Tanzania,Jimbo la Kusini Magharibi,usharika wa Ruanda mjini Mbeya.Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Rungwe,Mh. Cripin Meela.
Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimuhamasisha mmoja wa waalikwa kuchangia katika harambe ya kuchangia ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike katika Chuo Kikuu cha
Teofilo Kisanji, kinachomilikiwa na Kanisa la Moravian nchini
Tanzania,Jimbo la Kusini Magharibi,usharika wa Ruanda mjini Mbeya.
Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (wa pili kushoto) akifurahia jambo wakati alipokuwa katika Mazungumzo na Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania (KMT), Askofu Alinikisa Cheyo (kushoto) wakati wa hafla ya harambe ya kuchangia ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike katika Chuo Kikuu cha
Teofilo Kisanji, kinachomilikiwa na Kanisa la Moravian nchini
Tanzania,Jimbo la Kusini Magharibi,usharika wa Ruanda mjini Mbeya..
Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiagana na viongozi mbalimbali wa Chuo hicho mara baada ya kuongoza harambe ya kuchangia ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike katika Chuo Kikuu cha
Teofilo Kisanji, kinachomilikiwa na Kanisa la Moravian nchini
Tanzania,Jimbo la Kusini Magharibi,usharika wa Ruanda mjini Mbeya.

Tuesday, July 17, 2012

RAIS KIKWETE AMKARIBISHA RAIS WA LIBERIA IKULU LEO!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete na mgeni wao Rais Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia alipowasili Ikulu jijini Dar es salaam leo kwa maongezi rasmi pamoja na dhifa ya kitaifa. PICHA NA IKULU.

Emirates Offers Tanzania Travellers Special Ramadan Fares

Emirates has unveiled a range of great value Economy Class fares from Dar es Salaam to more than 50 destinations across the Middle East, Europe, the Indian Subcontinent, Far East and Asia during the month of Ramadan.

Economy Class return fares from Dar es Salaam to Dubai now start from US$ 670 and Business Class fares from US$ 1840 during the time-limited offer period. Bookings must be made by 31st July for travel between 15th July and 15th August 2012.


Announcing the new promotional fares in Dar es Salaam, Emirates Country Manager for Tanzania Abdul-Aziz Al Hai said: “As we approach the Ramadan period, we would like to make it as easy and convenient as possible for our customers to spend precious time with family and friends, or to enjoy a well-deserved vacation. These offers provide an opportunity to travel to a wide number of popular destinations at greatly discounted fares and we invite all our customers to take advantage of these fantastic value-for-money deals.”


Special Economy Class offers for the Middle East and Asia include: Bahrain from US$ 557; Kuwait from US$ 550; Muscat from US$ 556; Doha from US$ 560; Riyadh from US$ 562; Dammam from US$ 562; Islamabad, Karachi, Peshawar and Lahore S$ 970; Cochin, Kozhikode, Chennai, and Kolkata from US$725; Colombo from US$ 1135; Dhaka from US$ 955; Thiruvananthapuram from US$ 735; Hyderabad from US$758; Mumbai from US$730; Ahmedabad from US$733; Bengaluru from US$741; and New Delhi from US$801.


Economy Class deals to Europe include London Heathrow from US$ 1010; London Gatwick from US$ 975; Birmingham from US$ 972; Manchester from US$ 977; Dublin from US$ 855; Newcastle from US$ 977; Glasgow from US$ 972; Paris from US$ 892; Zurich from US$ 872; Geneva from US$ 851; Milan from US$ 850; Nice from US$ 870; Barcelona from US$ 843; Malta from US$ 852; Athens from US$ 851; Rome from US$ 851; Venice from US$ 850, Munich from US$ 912; Vienna from US$ 905; Frankfurt from US$ 928; Prague from US$ 855; and Dusseldorf from US$ 906. Others include Amsterdam from US$ 866; Hamburg from US$ 890; Copenhagen from US$ 855; St Petersburg from US$ 860; Moscow from US$ 852; Istanbul from US$ 843; Lisbon from US$ 856; Larnaca from US$ 860; and Madrid from US$ 866.


Emirates is also offering discounted Business Class return fares from US$ 2420 to Karachi, Peshawar, Lahore and Islamabad; US$2205 to Kolkata, Cochin, Kozhikode, and Chennai; US$ 2213 to Ahmedabad and Hyderabad; US$ 2480 to Colombo; US$ 2215 to Thiruvananthapuram; US$ 2221 to Bengaluru; and US$2281 to New Delhi.

MKURUGENZI WA MAMBO YA KALE BW. DONATIUS KAMAMBA ATEULIWA KUWA MJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI YA ICOMOS!

Bw. Donatius Kamamba, Mkurugenzi wa Mambo ya Kale katika Wizara ya Maliasili na Utalii , ameteuliwa kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirika la Kimaifa lisilo la Kiserikali liitwalo The International Council on Monuments and Sites - ICOMOS” kwa kipindi cha miaka mitatu (3) hadi Novemba, 2014. Uteuzi huo ulifanywa na Gustavo Araoz, Rais wa ICOMOS tarehe 3 Julai, 2012.

ICOMOS ni Shirika la Kimataifa lisilo la kiserikali lenye jumla la nchi wanachama 98. Majukumu yake ni pamoja na kutoa ushauri kwa UNESCO kuhusu Uhifadhi wa Urithi wa Utamaduni na hufanya tathmini ya maeneo yanayopendekezwa kuingizwa kwenye Orodha ya Urithi wa Utamaduni - World Heritage Sites. Aidha, ICOMOS inalo jukumu la kutathmini shughuli za uhifadhi zinavyotekelezwa katika maeneo ambayo tayari yapo katika Orodha ya Urithi wa Utamaduni.


Kuteuliwa Bw. Donatius Kamamba kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya ICOMOS ni ishara kuwaTanzania inayo taaluma katika fani ya Uhifadhi wa Urithi wa Utamaduni na inayatunza vizuri maeneo husika yaliyoko nchini. Maeneo hayo ambayo ni vivutio vya utalii ni kama vile: Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songomnara, Michoro ya miambani ya Kondoa, Eneo la Bonde la Oldupai, Nyayo za Zamadamu zilizoko Letoli, Miji ya Kihistoria ya Pangani, Kilwa Kivinje na Mikindani, Majengo ya kihistoria ya Ikulu , Maboma ya Kijerumani ya Biharamlo na Mahenge na Njia ya Kati ya biashara ya Utumwa.


Aidha Bwana Kamamba anazo nyadhifa nyingine za kimataifa. Mwaka 2007 alichaguliwa kuwa mjumbe wa Baraza la Uongozi wa Kituo cha Kimataifa cha Mafunzo ya Uhifadhi wa Urithi wa Rasimali za Utamaduni (International Centre for the Study of Preservation and Restoration of Cultural Property - ICCROM), kilichopo Roma, Italia. Pia mwaka jana Novemba, 2011, aliteuliwa kuwa Rais wa nchi wanachama wa ICCROM kwa kipindi cha miaka miwili Novemba ,2001 mpaka Novemba, 2013.

ALLY REHMTULLAH'S COLLECTION AT THE TRENDZ KENYA FASHION FESTIVAL 2012.





















Pictures by Thomson Ncube.

CARS FOR SALE "DISCOVERY 3'.








Interested please call Fawz +255784751762 or Khamisy on +255774540053email lucaskitojo@gmail.com

CAR FOR SALE 'MITSUBISHI SHOGUN 3.5 GDI WARRIOR 3DR AUTO SW SPECIAL EDS









MITSUBISHI SHOGUN WARRIOR GDI AUTO SILVER SHORT WHEEL BASE 3 Door Estate, Silver, Petrol, Automatic, Electrically adjustable drivers seat, Alloy wheels, Body coloured bumpers, Trip computer, Rear wiper, Heated front seat. EXCELLENT CONDITION,  Safety Features: 4-Wheel Drive, Alarm, Anti-Lock Brakes (ABS), Driver Airbag, Electronic Stability Program (ESP), Immobiliser, Passenger Airbag, Rear seat belts Year: 2003 Exterior: Alloy Wheels, Rear Spoiler, Tow Bar  Interior/Comfort Options: Air Conditioning, Climate Control, Cruise Control, Electric heated seats, Leather Seats,  Power Locks, Power Seats, Power Windows, Tilt Steering Wheel Engine Size: 3500 cc In-Car Audio: CD Player.

Interested please call Fawz +255784751762 or Khamisy on +255774540053email lucaskitojo@gmail.com 

THE CHOCOLATE CREW LAIBUKA MSHINDI SERENGETI DANSI LA FIESTA DAR, LAJINYAKULIA KITITA CHA MILIONI MOJA!









Kundi la The Chocolate Crew likishangilia kitita cha shilingi milioni moja mara baada ya kuibuka washindi kati ya makundi saba yaliyojitokeza kushiriki shindano la Serengeti dance la Fiesta 2012,ndani ya kiota cha maraha cha Suncirro,Sinza jijini Dar.Katika shindano hilo kulikuwepo na ushindani mkubwa lakini mwisho wa siku mshindi ilikuwa ni lazima ajulikane/apatikane.Shindano hilo ambalo mdhamini wake mkuu ni kampuni ya bia ya Serengiti ndio mdhamini mkuu wa tamasha kubwa lijalo la Fiesta linalorajiwa kuanza hapo baadae mara baada ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kuisha.Shindano la namna hii limekwishafanyika katika mkoa wa Arusha ambapo mshindi lilikuwa kundi la Contegious Crew,mkoani Tanga kundi la Questions Crew waliibuka washindi pamoja na Viswani Zanzibar ambapo kundi la B-Six lilishinda.Aidha makundi yote hayo yalijinyakulia kitita cha shilingi milioni moja.










Mmoja wa majaji na mratibu wa shindano hilo ajulikanae kwa jina la Msami akikabidhi kitita cha shilingi milioni moja kwa kundi la The Chocolate mara baada ya kuibuka kinara jioni ya leo kwenye ukumbi wa Sun Cirro,sinza jijini Dar.










 Baadhi ya mwashabiki wakishangilia










Mmoja wa watangazaji wa Clouds TV,Babu wa Kitaa kupitia kipindi Bibi Bomba akiwa amepozi na wadau wengine wa Clouds Media Group wakifuatilia shindano la Serengeti dance la Fiesta 2012.










Kundi la Mazabe Ndonga likionesha umahiri wa kucheza jukwaani kwenye shindano la kumsaka mshindi wa Serengeti dance la Fiesta 2012,ndani ya kiota cha maraha cha Suncirro,Sinza jijini dar.Katika shindano hilo yamejitokeza makundi saba ambayo yameshindana vikali katika kumsaka kinara wao,zawadi katika shindano hilo ambalo mdhamini wake mkuu ni kampuni ya bia ya Serengi,ni fedha taslimu shilingi Milioni moja.Mashindano haya yamekwishafanyika katika mkoa wa Arusha ambapo mshindi lilikuwa kundi la Contegious Crew,Zanzibar likashinda kundi la B-Six na mkoani Tanga kundi la Questions Crew waliibuka washindi,aidha makundi yote hayo yalijinyakulia kitita cha shilingi milioni moja.










Mmoja wa wasanii wa kundi la The Ridder akionesha mbwembwe zake kwa mashabiki kibao (hawapo pichani) waliofika kwenye shindano hili jioni ya leo,ambalo lilikuwa na msisimko mkubwa .













 Kundi la Tatanisha Dancers likisaka ushindi kwa udi na uvumba.












Baadhi ya washabiki waliojitokeza jioni ya leo kwenye shindano la kumsaka mshindi wa Serengeti dance la Fiesta 2012,ndani ya kiota cha maraha cha Suncirro,Sinza jijini dar










Mmoja wa majaji wa shindano hilo Isakwisha Thomson kutoka Clouds FM akifafanua jambo,kati ni Msami kutoka THT pamoja na B-Dozen kutoka Clouds FM,Wote ndio waratibu wa shindano hilo la Serengeti dance la  Fiesta 2012.










Kundi la Manzese Crew  likisaka ushindi kwa udi na uvumba jukwaani kuwania kitita sh milioni moja. 










 Mashabiki wakifuatilia shindani hilo jioni ya leo.










 Kundi la Chocolate lionesha mbwembwe zake jukwaani kuwani kitita cha shilingi milioni moja.










 Mmoja wa majaji katika mashindano hayo Isakwisa Thomson akielezea jambo wakati shindano likiendelea.










 Mc wa shindano zima,Nickson akiwayataja makundi yaliyotinga fainali kwenye mchakato wa kulipata kundi kinara la Serengeti dance la Fiesta 2012.










 Majaji wakijadiliana jambo kumpata mshindi










Palikuwa hapatoshi jioni ya  leo ndani ya ukumbi wa maraha wa Sun Cirro,Sinza jijini Dar.

NCHI ZAIDI ZA AFRIKA ZAJIUNGA NA APRM

      Katibu Mtendaji wa APRM, Rehema Twalibu akitambulisha ujumbe wa wataalam wa APRM

Na Mwandishi Wetu,Addis Ababa
Mataifa zaidi ya Afrika yamesaini mkataba wa kujiunga na mchakato wa Afrika Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM) wakati wa kikao cha wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika (AU) zinazoshiriki katika tathmini ya APRM mjini hapa.
Mkutano wa wakuu wa nchi zinazoshiriki APRM ulifanyika Jumamosi ikiwa ni siku moja kabla ya kuanza kwa kikao cha wakuu wa nchi za AU ambapo Rais Jakaya Kikwete aliongoza idadi ya Marais wa Afrika waliohudhuria mkutano huo wa APRM.


Nchi mpya zilizosaini mkataba wa kukubali kukaguliwa kiutawala bora chini ya APRM ni Niger, Cape Verde, Chad, Tunisia na Guinea ya Ikweta, hivyo kufikisha idadi ya nchi 36 kati ya 54 wanachama wa AU walioamua kujiunga na mchakato wa APRM.


Kwa mujibu wa Ofisa Habari na Mawasiliano wa APRM Tanzania, Hassan Abbas, APRM huipa nchi fursa kuanzisha taasisi yake ya ndani kwa lengo la kuwapa wananchi fursa ya mara kwa mara kuitathmini nchi yao katika utawala bora, kisha tathmini hiyo kuhakikiwa na wataalamu wengine kutoka nchi za Afrika kwa lengo la Afrika kama Bara na kila nchi kujikosoa ili baadaye kujisahihisha.


Akizungumza mjini Addis mara baada ya mkutano huo wa marais, Katibu Mtendaji wa APRM Tanzania, RehemaTwalib alisema mkutano huo ulikuwa wa mafanikio na viongozi hao walipitisha maazimio mengi ikiwemo kuiimarisha APRM ili kuwa taasisi kamili ya Umoja waAfrika.


Rais Kikwete aliunganana marais wengine akiwemo Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Waziri Mkuu wa Ethiopia,Melesi Zenawi na Rais wa Uganda Yoweri Museveni katika mkutano huo.


Mkutano huo pamoja namambo mengine pia ulijadili taarifa ya utekeleza wa hali ya utawala bora kwa nchiza Uganda, Burkina Faso na Algeria. Rais Abdulaziz Bouteflika wa Algeria aliwakilishwa na Waziri Mkuu wan chi hiyo, Ahmed Ouyahia.


Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika zilizojiunga mapema tu tangu mchakato huo ulipoanzishwa mwaka 2003 kwa kusaini mkataba mwaka 2004, Bunge likauridhia mwaka 2005 na tayari ripoti iliyosheheni maoni ya Watanzania kuhusu utawala bora nchini imeshakamilika.

UNAJUA KWAMBA MILLARD AYO ALIWAHI KUTOLEWA KATIKA CHUMBA CHA MTIHANI KWA KUTOMALIZIA ADA?

Kama tulivyokuahidi msomaji wa Mo blog ifuatayo ni sehemu ya pili ya mahojiano kati ya Mhariri wa Mo Blog Lemmy Hipolite na Mtangazaji maarufu Millard Ayo.



Mo Blog: Tunamsikia Millard Ayo lakini hatujui ni nani hasa.?

Millard Ayo: Milliard Ayo ni kijana wa miaka 26 aliyezaliwa tarehe 26 Januari mwaka 1986 ni kijana aliyezaliwa katika hospitali ya Mount Meru na ni mtoto wa kwanza kwenye familia ya watoto wanne.

Ninatoka katika familia ya Mzee Arael Ayo al maarufu kama ‘Chalii’ pale Tengeru mkoani Arusha.

Mo Blog: Tupe siri ya mafanikio yako pamoja na umaarufu ulionao.?


Millard Ayo: Kiukweli moja kati ya vitu vinavyonifanya mimi nipate mafanikio, namshukuru Mungu kwa sababu kwanza situmii vitu vinavyowaangusha watu wengi kwenye kazi kama hizi; kwanza kabisa mimi sinywi pombe na sijawahi kunywa tangu nizaliwe; nadhani inanisaidia pia kwa sababu wakati wote akili inakuwa ‘fresh’.

Mo Blog: Kwa kifupi tuambie ilikuaje mara ya mwisho tumekusikia Radio One ghafla Clouds FM.?


Millard Ayo: Clouds Fm walivutiwa na kazi yangu, nadhani waliona uwezo wangu kupitia show ya ‘Milazo 101’ niliokuwa nikiifanya Radio One so alinipigia simu bosi wao nakumbuka ilikuwa ni siku ya Jumatano akaniambia tuonane.


Ukizingatia mimi nilikuwa na dream sana kufanya kazi ‘Clouds’ hata wakati naingia college ya Journalism nilikuwa na ndoto za kufanya kazi Clouds.


Kuendelea kusoma mahojiano haya zaidi ingia humu, www.mohammeddewji.com/blog

BHAKRESA AWA MTEJA WA KWANZA KUNUNUA GARI MPYA AINA YA 'VOLKS WAGON AMAROK' NCHINI


Haya ndio Magari Mawili aina ya 'VOLKS WAGON AMAROK' yaliyonunuliwa na Mfanyabiashara maarufu nchini Said Bhakresa.

Pichani Juu na Chini ni Afisa Mauzo wa Kampuni ya Alliance Autos (T) LTD inayouza magari hayo Bw. Julius Guni(kushoto) akimkabidhi Funguo pamoja na Manual Book za magari hayo mwakilishi wa mzee Bhakresa Bw. Omar Said kutoka Bhakresa Food Products.



Bw. Omar Said katika pozi baada ya kukabidhiwa rasmi magari hayo.



Bw. Omar Said akichomeka funguo kuwasha moja ya magari hayo.



Wow.....Kweli ni 'VOLKS WAGON AMAROK'.

Volks Wagon 'Amarok' za Mzee Bhakresa.

Mwakilishi kutoka kampuni ya Bhakresa Food Products Bw. Omar Said akikagua Injini ya moja wapo ya gari hizo sambamba na Afisa Mauzo wa Kampuni ya Alliance Autos (T) LTD Bw. Julius Guni.
Mkurugenzi mpya wa kampuni mpya ya Alliance Autos (T) LTD Bw. Alfred Minja akiwajibika ofisini kwake kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa na wateja wanapata taarifa za kutosha kuhusiana na kampuni hiyo pamoja na magari wanayouza.
Kanpuni hiyo imeanza kazi rasmi tarehe 1 Julai mwaka huu chini ya Mkurugenzi huyo mpya na tayari leo tarehe 11 Julai wamefanikiwa kuuza magari mawili aina ya 'VOLKS WAGON AMAROK'.
Pichani Juu na Chini ni Fundi wa Kampuni ya Alliance Auto (T) LTD Bw. Dennis Dismas akifanya Services ya Magari ya Wateja wa Kampuni hiyo kwa Teknolojia ya kisasa inayotumia Kompyuta.

Mzigo wa kutosha wa magari aina ya 'VOLKS WAGON AMAROK' katika yadi ya kampuni ya Alliance Autos (T) LTD iliyopo barabara ya Pugu/Nyerere jijini Dar es Salaam.